ALFAJIRI
Ee Mungu na Bwana wangu! Mimi ni mutumishi Wako na Mwana wa mtumishi Wako. Nimeamka kutoka kitandani mwangu kwenye mapambazuko haya wakati Nyota ya Mchana ya umoja Wako imemulika kutoka Mapambazuko ya amri yako, na imetoa mng’ao wake juu ya ulimwengu wote, kulingana na yale yaliyoamriwa katika Vitabu vya Amri Yako.
Sifa iwe Kwako, Eee Mungu wangu, kwamba tumeamka kwenye wangavu wa nuru ya maarifa Yako. Tushushie basi, Ee Bwana wangu, kitakachotuwezesha kutomtaka yeyote ila Wewe, na kitakachotuondolea mshikamano wote kwa chochote ila Wewe. Andika, tena, kwa ajili yangu, na kwa ajili ya wale walio wapendwa wangu, na kwa ajili ya jamaa zangu, mwanaume na mwanamke sawa, mema ya ulimwengu huu na ulimwengu ujao. Kisha utuweke salama, kupitia ulinzi Wako usioshindwa, Ee Wewe Uliyempendwa wa viumbe wote na Shauku ya malimwngu yote, kutokana na wale ambao Umewafanya kuwa wadhihirishaji wa mnong’onezaji muovu, ambaye hunong’ona katika vifua vya watu. Wewe una nguvu kufanya utakavyo. Wewe kweli, ndiye Mwenyezi Msaada katika Shida, Aliyepo Mwenyewe.
Mbariki, Ee Bwana Mungu wangu, Yeye Ambaye Umempa majina Yako bora kabisa, na ambaye kupitia kwake Wewe umewagawanya wamchao Mungu na waovu na utusaidie kwa rehema, tufanye Ulitakalo na Ulitamanilo. Wabariki, tena, Ee Mungu wangu, wao ambao ni Maneno Yako na Herufi Zako, na wale ambao wamekazia nyuso zao kuelekea Kwako, na kugeukia kwenye uso Wako na kuitika kwenye Mwito Wako.
Wewe hakika, ndiye Bwana na Mfalme wa watu wote na una nguvu juu ya vitu vyote.