Ridván Messages
Swahili · Universal House of Justice
Mwaka wa maandalizi na tafakari, hali kadhalika wa juhudi kubwa, umehitimishwa, ukipambanuliwa kwa jitihada za marafiki kote ulimwenguni kuashiria miaka mia moja ya Kupaa kwa ‘Abdu’l-Bahá, zikijumuisha utumaji wa wawakilishi kushiriki katika tukio maalum la kumuenzi Yeye katika Nchi Takatifu. Kupitia jitihada hizi, uvuvio uliotolewa na maisha ya ‘Abdu’l-Bahá umehisiwa na roho zisizo na idadi na si tu Wabahá’í. Kumjali Kwake kila mwana-familia wa jamii ya wanadamu, kazi Yake ya ufundishaji, uendelezaji Wake wa shughuli za elimu na usitawi wa kijamii, michango Yake ya kina kwenye mijadala kote Magharibi na Mashariki, utiaji Wake moyo wa dhati wa miradi ya kujenga Nyumba za Ibada, uundaji Wake wa mwanzoni wa miundo ya utawala wa Kibahá’í, ukuzaji Wake wa sura mbalimbali za maisha ya jumuiya—sura zote hizi zinazoshamirishana za maisha Yake zilikuwa taswira za kujitoa Kwake kwa daima na kikamilifu kwenye kumtumikia Mungu na kuitumikia jamii ya wanadamu. Mbali na kuwa kinara wa kutegemewa wa mamlaka ya kimaadili na umaizi wa kiroho wa hali ya juu, ‘Abdu’l-Bahá alikuwa njia isiyo na doa ambayo kwayo nguvu zilizoachiliwa na Ufunuo wa Bahá’u’lláh zingeweza kutenda kazi juu ya ulimwengu. Ili kutambua nguvu ya ujengaji jamii ambayo Imani inayo, mtu hahitaji kuangalia mbali zaidi kuliko mafanikio ya ‘Abdu’l-Bahá wakati wa utumishi Wake na matokeo yabadilishayo ya miongozo iliyotiririka bila kukoma kutoka kwenye kalamu Yake. Maendeleo mengi sana ya kushangaza yaliyofanywa na jumuiya ya Kibahá’í ya sasa--ambayo yalitazamwa katika ujumbe wetu kwenu wa Riḍván iliyopita—hufuatilia vyanzo vyake kwenye vitendo, maamuzi na maelekezo ya ‘Abdu’l-Bahá.
Ni ya kufaa namna gani, basi, kwamba shukrani za pamoja za jumuiya ya Kibahá’í kwa Mfano wake mkamilifu inavyopaswa kuunda mwanzo wa uanzishwaji wake wa shughuli kuu ikimakinikia juu ya uachiliaji wa nguvu ya Imani ya ujengaji jamii kwa viwango vikubwa zaidi. Maeneo ya jitihada ambayo huangukia ndani ya uwanda wa Mpango wa Miaka Tisa, na wa mfululizo wa sasa wa Mipango, inaelekezwa kwenye utimizaji wa shabaha hii kuu. Pia ni shabaha ya zaidi ya makongamano 10,000 yanayofanyika kote duniani kuashiria uzinduzi wa shughuli hii kuu ya kiroho. Makongamano haya, yanayotarajiwa kukaribisha idadi isiyo na mfano ya washiriki, siyo tu yawaleta pamoja Wabahá’í bali pia watakia heri wengine wengi wa jamii ya wanadamu ambao hushiriki nao shauku ya kukuza umoja na kuboresha ulimwengu. Dhamira yao na hisia yao thabiti ya kusudi vinaakisiwa katika moyo uliofanyizwa kwenye mikusanyiko ambayo tayari imekwishatokea, ambapo washiriki wameamshwa sana kwa ushauriano wenye nguvu ambao wamechangia kwa muono wa pamoja uliochunguzwa kwenye matukio haya ya shangwe. Tunatazama kwa matarajio makubwa kwa yale ambayo miezi na miaka ijayo itayaleta.
Tangu tulipotoa ujumbe wetu wa 30 Desemba 2021 kwa Kongamano la Washauri, Mabaraza ya Kiroho ya Kitaifa na Halmashauri za Kibaha’i za Kanda yamekuwa yakitathmini kwa shauku uwezekano wa kushadidisha mchakato wa ukuaji katika klasta zilizo ndani ya maeneo yao ya mamlaka katika kipindi cha Mpango wa Miaka Tisa. Tunahisi ingekuwa ya kufaa, kwa kusudi la kupima maendeleo yaliyofanyika kwa kipindi hicho, kuuona Mpango huu kama unaojikunjua katika awamu mbili za kipindi cha miaka minne na mitano, na Mabaraza ya Kitaifa yalialikwa kufikiria maendeleo wanayoyatarajia kuyaona katika jumuiya zao husika ifikapo Riḍván 2026 na kisha ifikapo Riḍván 2031. Zoezi hili pia lilihusisha kutathminiwa upya kwa mipaka ya klasta, na matokeo ya marekebisho haya ni kwamba jumla ya idadi ya klasta ulimwenguni imepanda kwa robo na sasa ipo zaidi ya 22,000. Kwa kutegemea matabiri yaliyopokelewa, inakadiriwa kwamba, ifikapo mwisho wa Mpango, programu za ukuaji kwa kiwango fulani cha maendeleo zitakuwepo katika takribani klasta 14,000 kati ya hizi. Kutoka miongoni mwa hizo, idadi ambazo programu ya ukuaji ingeweza kufikiriwa kuwa shadidi inakisiwa kupanda hadi kufikia 11,000 katika kipindi hicho hicho. Na kati ya hizi, inatazamiwa kwamba idadi ya klasta ambamo hatua ya tatu ya ukuaji itakuwa imevukwa itapanda zaidi ya 5,000 ifikapo 2031. Pasipo swali, ili kupiga hatua kama hizo zitahitajika jitihada kubwa mno kwa kipindi chote cha Mpango. Bado tunaona haya kuwa ni matarajio ya kupambania, kwani yanawakilisha tathmini yenye nia kuu lakini ya dhati ya kile kilicho ndani ya uwezo wa kufikiwa.
Hiki ndicho kinachosemwa. Shabaha kama hizo zisingeweza kufikiriwa kiuhalisia kama asasi za kiutawala na mawakala zisingekuwa zimekua dhahiri, kuzijalia uwezo utambulikao uliokuzwa kusimamia mambo ya jumuiya ambazo shughuli zake zimeongezeka kwa haraka, zikikumbatia idadi kubwa na ikuayo ya roho ndugu. Isingewezekana kutarajia ukuaji wa namna hiyo kama shauku ya kujifunza—kutenda, kutafakari, kuchota umaizi na kufyonza umaizi unaoibuka kwingineko—isingekuwa imekuzwa kwenye ngazi zote, kufikia kwenye ngazi ya umma ya jumuiya. Na jitihada imaanishwayo kwa makadirio kama hayo isingewezekana kama mbinu za kimpangilio kwenye kazi ya ufundishaji na kwenye ukuzaji wa rasilimali watu isingekuwa imeendelea kuwa dhahiri katika ulimwengu wa Kibahá’í. Yote hii imeleta ongezeko la utambuzi katika jumuiya ya Kibahá’í wa utambulisho na kusudi lake. Dhamira ya kuwa na mtazamo wa nje katika mchakato wa ujengaji jumuiya tayari ilishakuwa sehemu madhunuti ya utamaduni katika maeneo mengi, mengi; sasa imeshamiri, katika idadi iongezekayo ya jumuiya, katika hisia ya jukumu halisi kwa ajili ya maendeleo ya kiroho na ya kimwili ya makundi makubwa na makubwa zaidi katika jamii, mbali zaidi ya uumini wa jumuiya ya Kibahá’í yenyewe. Jitihada za marafiki kujenga jumuiya, kujihusisha katika shughuli za kijamii, na kuchangia kwenye mijadala inayoendelea ya jamii zimeunganika katika shughuli moja ya kiulimwengu, zikifungamana kwa pamoja kwa muundo wa pamoja wa utendaji, ukilenga juu ya kusaidia jamii ya wanadamu kuanzisha mambo yake juu ya msingi wa kanuni za kiroho.
Umuhimu wa maendeleo tuliyokwishayaelezea, kufikia hatua hii miaka mia moja baada ya uzinduzi wa Utaratibu wa Utawala, hauwezi kupuuzwa. Katika ongezeko lisilo la kawaida la uwezo lililotokea katika miongo miwili iliyopita—na ambao umewezesha ulimwengu wa Kibahá’í kutazama jitihada zake kwa maana ya uachiliaji wa nguvu ya Imani ya ujengaji jamii—tunaona ushahidi usiopingika kwamba Hoja ya Mungu imeingia kipindi cha sita cha Zama yake ya Ujenzi. Riḍván iliyopita tulitangaza kwamba hali iliyoenea ya idadi kubwa inayoshiriki katika shughuli za Kibahá’í, ikiwashwa kwa imani, na ikijitwalia ujuzi na uwezo mwingi kuhudumia jumuiya zao iliashiria kwamba kipindi cha tatu cha Mpango Mtakatifu wa Bwana kilikuwa kimeanza; hivyo, Mpango wa Mwaka Mmoja, kwenye mwanzo wake wakati ule na kwenye hitimisho lake sasa, umekuja kuashiria maendeleo kadhaa ya kihistoria yaliyofanywa na kundi la waaminifu. Na kwenye kizingiti cha shughuli kuu mpya, shirika hili lililounganika la waumini lipo tayari kutwaa fursa zilizo wazi mbele yake.
Sura inayojitokeza ya kipindi kinachomalizika sasa ilikuwa ni ujenzi wa Nyumba za mwisho za Ibada za kibara na uanzishwaji wa miradi ya kujenga Nyumba za Ibada kwenye ngazi za kitaifa na mahali. Mafunzo mengi yamepatikana, na Wabahá’í kote ulimwenguni, kuhusu dhana ya Mashriqu’l-Adhkár na muunganiko wa ibada na huduma inavyovijumuisha. Wakati wa kipindi cha sita cha Zama ya Ujenzi, mengi zaidi yatapatikana kuhusu njia ambayo huongoza kutoka maendeleo ndani ya jumuiya yenye maisha ya ibada yanayoshamiri—na huduma ambayo huivuvia—hadi utokezaji wa Mashriqu’l-Adhkár. Mashauriano yanaanza na baadhi ya Mabaraza ya Kiroho ya Kitaifa, na haya yakiendelea, tutawatangazia kila baada ya kipindi fulani mahali ambako Nyumba za Ibada za Kibahá’í zitajengwa katika miaka ijayo.
Furaha yetu ya kuona jumuiya ya Jina Kuu Kabisa ikienda kutoka nguvu hadi nguvu inapunguzwa na huzuni yetu kuu ya kuona ung’ang’anifu wa hali na mafarakano ulimwenguni ambavyo husababisha mateso yenye taabu na kutokuwa na matumaini—hususan, kuona kurudia kwa nguvu za uharibifu ambazo zimevuruga mambo ya kimataifa wakati zikipeleka vitisho kwa watu. Tunafahamu fika na tunahakikishiwa tena kwamba, kama jumuiya za Kibahá’í mara kwa mara tumeonesha katika miktadha mingi mbalimbali, wafuasi wa Bahá’u’lláh wamejidhatiti katika kuleta ahueni na msaada kwa wale wanaowazunguka, bila kujali hali zao ni za dhiki kiasi gani. Lakini mpaka pale jamii ya wanadamu kwa jumla itakapoamua kuweka mambo yake juu ya misingi ya haki na kweli, ole, imetabiriwa kuwa na misukosuko kutoka hali moja ya hatari hadi nyingine. Tunasali kwamba, ikiwa mlipuko wa sasa wa vita huko Ulaya utatoa mafunzo yoyote kwa ajili ya siku zijazo, itakuwa kama kumbusho la haraka la muelekeo ambao ulimwengu lazima uchukue kama unataka kufikia amani ya kweli na ya kudumu. Kanuni zilizotolewa na Bahá’u’lláh kwa tawala na marais wa kipindi Chake, na majukumu mazito ambayo Yeye aliagiza kwa watawala wa wakati uliopita na sasa, huenda yanafaa zaidi na ya muhimu leo kuliko yalipoandikwa kwa mara ya kwanza kwa Kalamu Yake. Kwa Wabahá’í, maendeleo yasiyozuilika ya Mpango Mkuu wa Mungu—ukiambatana na mateso na misukosuko, lakini hatimaye ukiisukuma jamii ya wanadamu kuelekea kwenye haki, amani na umoja—ni muktadha ambao ndani yake Mpango Mdogo wa Mungu, ambao waumini kwa kiasi kikubwa ndiyo wanaoshughulika nao, hukunjuka. Hali mbaya ya kiutendaji ya jamii ya sasa hufanya hitaji la uachilia nguvu ya Imani ya ujengaji jamii kuwa wazi kwa kiwango kikubwa na ya lazima. Hatuwezi bali kutegemea kwamba, kwa sasa machafuko na fujo vitaendelea kuutesa ulimwengu; bila shaka mtatambua, hivyo, kwa nini kila ombi la dhati tunalolitoa kwa ajili ya watoto wote wa Mungu kuachiliwa kutoka fadhaa na dhiki kali linaunganishwa sawia na sala ya dhati kwa ajili ya mafanikio ya huduma ihitajikayo sana mnayoitoa kwa ajil ya Hoja ya Mwana-Mfalme wa Amani.
Katika kila klasta ambako shughuli za Mpango zinapata msukumo, tunaona maendeleo ya jumuiya zenye tabia bora tulizozielezea katika ujumbe wa 30 Desemba 2021. Wakati jamii zikipitia mifadhaiko ya aina mbalimbali, wafuasi wa Uzuri wa Abhá lazima wajipambanue zaidi na zaidi kwa sifa zao za unyumbulikaji na urazini, kwa kiwango chao cha mwenendo na ushikiliaji wao wa kanuni, na kwa huruma, kujitenga na ustahimilifu wanazozionesha katika ufuatiliaji wao wa umoja. Mara kwa mara, tabia na mielekeo bainifu ioneshwayo na waumini katika nyakati za shida kali zimewasukuma watu kuwageukia Wabahá’í kwa ajili ya maelezo, ushauri na msaada, hasa pale maisha ya jamii yanapovurugwa na kukabiliwa na taabu na vikwazo visivyotabirika. Katika kushiriki chunguzi hizi, tunatambua kwamba jumuiya ya Kibahá’í yenyewe pia inapitia madhara ya nguvu za uchangukaji zilizo kazini katika ulimwengu. Zaidi, tunatambua kwamba kadiri jitihada za marafiki za kutangaza Neno la Mungu zilivyo kuu zaidi, ndivyo nguvu za ukinzani watakazokutana nazo zitakavyokuwa na nguvu zaidi, punde au baadaye, kutoka maeneo mbalimbali. Sharti waimarishe roho zao dhidi ya majaribu ambayo kwa hakika yatakuja, haya yasije yakatatiza uadilifu wa jitihada zao. Lakini waumini wanafahamu fika kwamba dhoruba zozote zilizo mbele yao, safina ya Hoja ni sawa kwao wote. Hatua zinazofuatana za safari yake zimeshaviona vidokezo vya hali ya hewa na wanakwea juu ya mawimbi. Sasa inaelekea kwenye upeo mpya. Mathibitisho ya Mwenyezi ndiyo dhoruba zinazojaza matanga yake na kuisukuma kuelekea mwisho wa safari yake. Na Agano ndiyo nyota yake iiongozayo, ikikiweka chombo kitakatifu kielekee kwenye uelekeo wake wa uhakika na yakini. Acha wakazi wa mbinguni watume baraka juu ya wote wasafirio ndai yake.
Tunahisi furaha kubwa mno kuwa tunaongea na jumuiya ambayo msimamo na azma yake ya juu hustahili wito wake mkuu. Ni mkubwa kiasi gani, ni mkubwa sana kiasi gani upendo wetu kwenu, na jinsi gani roho zetu zinavyopaa kadiri tunavyoona jitihada zenu za dhati na kujitoa kuishi maisha yanayobumbwa na Mafundisho ya Bahá’u’lláh na kutoa maji yatiayo uzima ya Ufunuo Wake kwa ulimwengu ambao una kiu sana. Hisia yenu kali ya kusudi inaonekana wazi. Upanuzi na uimarishaji, shughuli za kijamii, na ushiriki katika mijadala ya kijamii vinaendelea kwa kasi, na upatano wa kiasili wa shughuli hizi kwenye ngazi ya klasta daima unazidi kuonekana dhahiri. Hakuna popote ambapo hili huonekana wazi zaidi kuliko katika maeneo ambako idadi ziongezekazo zinaanza kujihusisha katika safu za jitihada, kila moja ikiwa njia ya kuachilia nguvu ya Imani ya ujengaji jamii.
Katika miezi kumi na mbili iliyomalizika tangu kuanza kwa Mpango wa Miaka Tisa, tumefurahishwa kuona jinsi shughuli hii ya kiroho ya ulimwengu ilivyowavuvia na kuwaamsha marafiki na kuwapa msukumo kwenye maeneo mahsusi ya utendaji. Hatua ya haraka ya kumakinikia imekuwa ni kuweka katika vitendo mipango ambayo huhakikisha kwamba, katika kila nchi na kanda, huibuka angalau klasta moja ambapo hatua ya tatu ya ukuaji imevukwa: mahali ambako idadi kubwa ya watu hufanya kazi kwa pamoja na huchangia kwenye maisha ya jumuiya hai. Wakitambua, hata hivyo, kwamba lengo kwa kipindi hiki cha miaka ishirini na tano ni kuanzisha program ya ukuaji shadidi katika kila klasta ulimwenguni, waumini pia wamejiandaa juu ya ufunguaji wa klasta mpya kwa Imani hali kadhalika kushadididsha juhudi zao katika maeneo ambayo tayari yana program ya ukuaji. Kuna utambuzi uliokuzwa wa fursa kwa ajili ya watangulizi kuinuka katika sehemu zote za ulimwengu—roho nyingi zilizojitoa zinafikiria jinsi zinavyoweza kuitikia fursa hii, na zingine nyingi tayari zimeshafanya hivyo, hili linaonekana dhahiri zaidi kwenye uwanja wa nyumbani lakini zaidi katika uwanja wa kimataifa vile vile. Hii ni mojawapo ya njia kadhaa ambamo, kama tulivyotumaini, moyo wa kusaidiana unadhihirishwa na marafiki kila mahali. Jumuiya ambako nguvu imejengwa zimejidhatiti zenyewe kusaidia maendeleo yanayofanywa katika eneo tofauti—katika klasta, kanda, nchi au hata bara lingine— na njia za kiubunifu zimepatikana ili kutoa hamasa kutokea mbali na kuwezesha tajiriba kushirikishwa moja kwa moja. Wakati huo huo, mbinu ya kimsingi ya kutwaa kile wanachojifunza katika klasta, ili kwamba kiweze kufahamisha mipango inayofanywa ndani na kwingineko, inatumika kwa mapana. Tumependezwa kuona kwamba umakini mahsusi unatolewa kwenye ujifunzaji wa jinsi ya kukuza ubora wa tajiriba ya kielimu itolewayo na taasisi. Wakati mchakato wa taasisi ukiota mizizi katika jumuiya, matokeo yake ni ya kuvutia. shuhudieni, mathalani, vile vituo vya shughuli shadidi ambako wakazi wamekuja kuichukulia taasisi ya mafunzo kama chombo chenye nguvu ambacho ni chao: chombo ambacho maendeleo yake thabiti wameyachukulia kama jukumu lao kuu. Wakijua vyema kwamba milango ya Imani daima ipo wazi, waumini wanajifunza jinsi ya kutoa hamasa kwa wale ambao wapo tayari kuingia. Kutembea na roho kama hizo, na kuzisaidia kuvuka kizingiti, ni upendeleo na shangwe maalum; katika kila muktadha wa kiutamaduni, kuna mengi ya kujifunza kuhusu nguvu za wakati huu wenye mvumo wa utambuzi na hisia ya kuwa sehemu yake. Na si hayo tu. Wakati katika klasta nyingi juhudi za kuchangia kwenye mabadiliko ya kijamii zipo katika hatua zake za mwanzoni kabisa, Mabaraza ya Kiroho ya Kitaifa, daima yakisaidiwa kwa ustadi na Washauri, yanapambana kutaka kujifunza zaidi kuhusu jinsi juhudi hizi zinavyoibuka kutoka kwenye mchakato wa ujengaji jumuiya. Majadiliano kuhusiana na usitawi wa kijamii na kimwili wa watu yanaendelezwa ndani ya makundi ya familia na katika jumuiya, wakati marafiki pia wanatafuta njia kushiriki katika mijadala ya maana ambayo inakunjuka katika mazingira yanayowazunguka.
Katikati ya yote tuliyoelezea, matendo ya vijana hung’aa kwa wangavu. Mbali na kuwa washarabu baridi wa ushawishi—uwe ushawishi unaofaa au vinginevyo— wamejithibitisha wenyewe kuwa washiriki jasiri na maizi wa Mpango. Pale ambapo jumuiya imewaona katika mtazamo huu na kutengeneza mazingira kwa ajili ya maendeleo yao, vijana wamethibitisha zaidi ya imani iliyooneshwa kwao. Wanafundisha Imani kwa marafiki zao na kuifanya huduma kuwa msingi wa urafiki wenye maana zaidi. Mara nyingi—huduma kama hiyo huchukua sura ya kuwaelimisha wale wadogo zao yao—wakiwapatia, siyo tu elimu ya kimaadili na kiroho, bali aghalabu msaada kwa masuala yao ya shule vile vile. Wakiwa na jukumu takatifu la kuimarisha mchakato wa taasisi vijana wa Kibahá’í wanatimiza matumaini yetu pendwa.
Mandhari ya juhudi zote hizi ni zama zilizovurugika sana. Kuna utambuzi ulioenea pote kwamba miundo ya sasa ya jamii inaandaliwa kwa hila kushughulikia mahitaji ya jamii ya binadamu katika taabu zake za sasa. Mengi ambayo yalidhaniwa kwa kiasi kikubwa kuwa ni ya uhakika na yasiyotetereka yanahojiwa, na matokeo ya mkoroganyo huo yanaleta shauku kwa ajili ya muono uunganishao. Kibwagizo cha sauti zilizopaazwa katika kuunga mkono umoja, usawa, na haki huonesha jinsi gani walio wengi hushiriki matamanio haya kwa ajili ya jamii zao. Bila shaka, haishangazi kwa muumini wa Uzuri Uliobarikiwa kwamba mioyo sharti itamani mambo ya kiroho yaliyo mema Aliyoyatoa. Lakini hata hivyo tunaona inavutia kwamba, ndani ya mwaka mmoja wakati matarajio kwa ajili ya maendeleo ya pamoja ya jamii ya binadamu mara chache yameonekana yenye ghamu; mwanga wa Imani uling’aa kwa wangavu wa kustaajabisha katika makongamano zaidi ya elfu kumi, yaliyohudhuriwa na takribani watu milioni moja na nusu, yakimakinikia juu ya njia za kuendeleza mambo hayo hayo mema. Muono wa Bahá’u’lláh, na rai Yake kwa jamii ya binadamu kufanya kazi kwa umoja kwa ajili ya uboreshaji wa ulimwengu ulikuwa ni kiini ambacho kwacho mambo anuwai ya jamii uliyakusanya kwa shauku—na haishangazi, kwani kama ‘Abdu’l-Bahá alivyoelezea, “Kila jumuiya ulimwenguni hupata katika Mafundisho haya Matakatifu utambuzi wa matamanio yake ya juu kabisa.” Baadhi ya watakia heri wa jamii ya binadamu mwanzoni wanaweza kuvutiwa kwenye jumuiya ya Kibahá’í kama mahali pa kimbilio, hifadhi kutoka ulimwengu uliogawanyika na kupooza. Bado, mbali na hifadhi, wanachokikuta ni roho ndugu zikifanya kazi kwa pamoja kuujenga upya ulimwengu.
Mengi yanaweza kuandikwa kuhusu ueneaji wa kijiografia wa makongamano haya, msukumo huu usio wa kawaida yaliyouingiza kwenye Mpango mpya, au sura za dhati za furaha na shauku yaliyoleta kutoka kwa wale waliohudhuria. Lakini katika mistari hii michache tunapenda kuelekeza kwenye kile yalichoashiria kuhusiana na maendeleo ya Hoja. Yalikuwa ni tafakari ya jumuiya ya Kibahá’í ambayo huona undugu, siyo tofauti. Muonekano huu ulifanya iwe kawaida kuchunguza Mpango wa Miaka Tisa kwenye mikusanyiko ambayo kwayo wote walikaribishwa. Marafiki walifikiria matokeo ya Mpango kwa ajili ya jamii zao siyo tu katika mwambatano wa watu binafsi na familia, bali viongozi wa maeneo na wenye mamlaka kadhalika. Kuwaleta pamoja watu wengi hivyo sehemu moja kulitengeza mazingira kwa ajili ya mazungumzo yabadilishayo kuhusu maendeleo ya kiroho na kijamii, yale yanayoukunjua ulimwengu mzima. Mchango maalum ambao mikusanyiko kama hiyo—iliyokuwa wazi, ya kutia moyo, na yenye kusudi—waweza kutoa kwenye ruwaza ipanukayo ya maendeleo ya jumuiya katika klasta ni somo la thamani sana kwa asasi za Kibahá’í kulizingatia kwa siku zijazo.
Na hivyo kundi la waaminifu linaingia mwaka wa pili wa Mpango likiwa na mtazamo mpya na umaizi wa kina kwenye umuhimu wa kile linachotaka kukitimiza. Jinsi gani matendo mbalimbali huonekana yanapotazamwa kwa mtazamo wa nguvu ya ujengaji jamii yanayoiachilia! Matarajio haya yapanukayo huruhusu shughuli inayodumishwa kuonekana kama zaidi ya kitendo kilichotengwa cha huduma au kama mahali tu pa taarifa. Katika kila mahali, jitihada zinazofanyika hufunua ujifunzaji wa watu juu ya namna ya kubeba majukumu yaongezekayo kwa ajili ya kuongoza njia ya maendeleo yake yenyewe. Matokeo ya mabadiliko ya kiroho na kijamii hujidhihirisha yenyewe katika maisha ya watu kwa namna mbalimbali. Katika mfululizo uliopita wa Mipango, ingeweza kuonekana dhahiri kabisa katika uendelezaji wa elimu ya kiroho na ibada ya pamoja. Katika mfululizo huu mpya wa Mipango, umakinifu uongezekao huhitaji kutolewa kwa michakato mingine ambayo hutaka kuinua maisha ya jumuiya—kwa mfano, kwa kuboresha afya ya jamii, kutunza mazingira au kutumia kwa ufanisi zaidi nguvu ya sanaa. Kile kinachohitajika kwa ajili ya pande zote hizi zinazoshamirishana za usitawi wa jumuiya kusonga mbele, bila shaka, ni uwezo wa kujihusisha katika ujifunzaji wenye mpangilio katika maeneo yote haya—uwezo ambao huchota kwenye umaizi unaoibuka kutokana na Mafundisho na hifadhi iliyokusanywa ya maarifa ya mwanadamu yaliyopatikana kupitia udadisi wa kisayansi. Kadiri uwezo huu ukuavyo, mengi yatatimizwa katika miongo ijayo.
Muono huu uliopanuliwa wa ujengaji jamii, una matokeo yanayofika mbali. Kila jumuiya ipo kwenye njia yake yenyewe kuelekea utambuzi wake. Lakini maendeleo katika sehemu moja yana sura zinazofanana na maendeleo katika sehemu nyingine. Sura moja ni kwamba, kadiri uwezo uongezekavyo na nguvu ya jumuiya ya mahali au kitaifa ziongezekavyo, basi, muda ukitimia, vigezo vihitajikavyo kwa ajili ya uibukaji wa Mashriqu’l-Adhkár, vilivyotajwa katika ujumbe wetu wa Riḍván 2012, hatimaye vitatimizwa. Kama tulivyoonesha katika ujumbe wetu kwenu Riḍván iliyopita, kila baada ya kipindi fulani tutabainisha maeneo ambako Hekalu la Kibahá’í litatakiwa kuinuliwa. Tunayo furaha kubwa kuagiza kwa wakati huu, usimikwaji wa Nyumba za Ibada za mahali huko Kanchanpur, Nepal, na Mwinilunga, Zambia. Zaidi ya hili, tunaagiza Nyumba ya Ibada ya kitaifa iinuliwe huko Canada, karibu karibu na Ḥazíratu’l-Quds ya Kitaifa iliyoanzishwa muda mrefu huko Toronto. Miradi hii, na mingine itakayoanzishwa hapo baadaye, itanufaika na msaada unaotolewa kwa ajili ya Mfuko wa Mahekalu kutoka kwa marafiki katika kila nchi.
Ni tele baraka ambazo Bwana mkarimu amechagua kuwajalia wapendwa Wake. Ni mtukufu wito, ni makubwa mno matarajio. Ni zenye uhitaji mno nyakati ambamo sote tumeitwa kuhudumu. Ni zenye hamasa, hivyo, sala ambazo kwazo, kwa niaba yenu na kwa juhudi zenu zisizochoka, tunasali kwenye Kizingiti cha Bahá’u’lláh.
Tsopano zaka ziwiri za ntchito yovuta zedi ya zaka zisanu ndi zinayi zatha. Abwenzi a Mulungu atengera pamtima kwambiri zolinga zake. Mu dziko lachiBahá’í monse pali kuzama kowonjezereka pa kumvetsetsa pa zomwe zikufunikira popitiliza kupititsa patsogolo ndondomeko yomanga dera ndi kusinthika kwa dera kwakukulu. Koma pakudutsa kwa tsiku lirilonse tikuona zinthu za m`dziko lapansi zikuvutira-vutira, kugawikana kukukulira-kulira. Mikangano yochuluka pakati pa anthu ndinso maiko ikukhudza anthu ndi malo munjira zochuluka.
Ichi chikusowekera yankho kuchokera kwa mzimu wina uliwonse wodalilika. Tonse tikuzindikira bwino lomwe kuti mbumba ya Dzina Lalikulu singayembekezere kukhala yosakhudzidwa ndi mavuto amenewa a dziko. Komabe, ngakhale ili yokhudzidwa ndi mavuto amenewa, sikuti yasokonezeka nawo; ndi yokhudzidwa ndi chisoni ndi kuvutika kwa mtundu wa anthu, koma sikuti yazingwa nawo. Kukhudzika kochokera pansi pamtima kuyenera kupangitsa kuchita kanthu mopitilira kumanga mbumba/madera amene angapereke chiyembekezo m`malo mwanjakata, kubweretsa umodzi pamene pali kukangana.
Shoghi Effendi anafotokoza momveka bwino momwe ndondomeko ya “kulowa pansi kopitilira kwa ntchito za anthu” ikuonekera molingana ndi ndondomeko ina, ndondomeko yolumikiza, nkudzera mwa iyo “Linga la chipulumutso cha munthu”, “pothawira pomaliza” pa dziko, likumangidwa. Ndife osangalala kuwona, mu dziko ndi chigawo china chilichonse, obweretsa mtendere owona ali otanganidwa ndi kumanga linga limeneli. Tikuona mu nkhani ina iliyonse mtima ukuyatsidwa ndi chikondi cha Mulungu, banja likutsegula khomo lake kwa abwenzi atsopano, ogwira ntchito limodzi akulunjika pa ziphunzitso za Bahá’u’lláh pofuna kuthana ndi mavuto a dera, mbumba imene ikulimbitsa khalidwe la kuthandizana, dera kapena mudzi ukuphunzira kuyambitsa ndi kupitiliza ntchito zofunikira pa kupita patsogolo kwake pauzimu ndinso kuthupi, dera likudalitsika ndi kukhazikitsidwa kwa Bungwe Lauzimu latsopano.
Njira ndi zida za Pulani zikuvomera mzimu wina uliwonse kusonkhera mbali ya chimene mtundu wa anthu ukufunika mu tsiku ili. Patali ndi kupereka thandizo la pompo lothetsa mavuto a nthawi yomweyo, ntchito za Pulani ndi njira imene ndondomeko zomanga za nthawi yayitali kudutsa mibadwo yochuluka zikukhadzikitsidwa dera lina lililonse. Zonsezi zikulunjika ku mathero osapeweka ndi a changu: Pakuyenera kukhala chiwerengero chachikulu, chopitilira cha iwo amene akupereka nthawi yawo, mphamvu zawo, ndi chidwi chawo ku chipambano cha ntchito imeneyi.
Ndi kutinso kwina, koma mu mfundo ya Bahá’u’lláh ya umodzi wa mtundu wa anthu, momwe dziko lapansi lingapeze masomphenya aakulu okwanira kuluzanitsa mbali zake zonse zosiyanasiyana? Angachite bwanjinso koposa kumasulira masomphenya amenewo mu dongosolo loyima pa umodzi mu kusiyana-siyana pomwe dziko lapansi lingachire ku mavuto a m’dziko amene aligawa ilo? Ndi ndani amene angakhale chotupitsa chimene kudzera mu icho anthu a dziko lapansi akhoza kupeza njira yatsopano ya moyo, njira yolunjika ku mtendere wosatha? Tambasulani choncho kwa wina aliyense dzanja la ubwenzi, la ntchito imodzi, la kutumikira kwapamodzi, la kuphunzira kwapamodzi, ndi kupita patsogolo ngati amodzi.
Tikuzindikira pamomwe kutaka-taka ndi mphamvu zikubwelera mu dera lina lililonse ndi achinyamata ake omwe akudzutsidwa ku masomphenya a Bahá’u’lláh ndikukhala atenga mbali a Pulani. Ndipo chomwecho, ndi kukoma mtima kozama, kulimba mtima ndi kudalira kotheratu pa Mulungu kumene achinyamata achiBahá’í ayenera kunyamuka ndi kufikira kwa amnzawo ndi kuwabweretsa mu ntchito iyi! Onse ayenera kusefukira, koma achinyamata akuyenera kutambasula mapiko awo ndi kuwuluka.
Changu cha ola ili chisatchinge chimwemwe chapadera chimene chimachokera mu kutumikira. Kuyitanidwa ku kutumikira ndi chinthu chokwezeka, chiyangato chachivomerezo. Kumakopa mzimu wokhulupirika uliwonse, ngakhale iyo imene ili yothodwa ndi zisamaliro ndi maudindo. Pakuti munjira zonse zimene mzimu wokhulupikawo watanganidwa nazo zitha kupezedwa mu kuzipereka kozama ndi kukhudzidwa kwa moyo wonse pa kuchita bwino kwa ena. Makhalidwe otere amapereka kukhala chikati-kati ku moyo wa zofuna zochuluka. Ndipo nthawi yotsekemera kwambiri pa zonse kwa mtima wina uliwonse woyatsidwa ndi imene umakhala limodzi ndi abale ndi alongo muuzimu, kutumikira ku zofunikira za dera limene likusowekera chakudya chauzimu.
Ku Malo Oyera, ndi mitima yosefukira, tikuthokoza Bahá’u’lláh pokudzutsani inu ndi kukuphunzitsani munjira Zake, ndipo tikupempha Iye kuti akutumizireni dalitso Lake.